Wed, 27 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Al Ahly imeanza safari kwa ndege binafsi kutoka nchini Misri kuja nchini kucheza mchezo wa robo fainali ya Ligi ya mabingwa Afrika dhidi ya Simba SC.
Klabu hiyo inatarajiwa kuwasili mchana leo na kuanza maandalizi ya moja kwa moja kwa ajili ya mchezo wa keshokutwa Ijumaa, Machi 29, 2024.
Tayari ujumbe wao wa kwanza uliwasili mapema nchini na kufanya maandalizi yao ya msingi kuipokea timu.
Simba ambao walikuwa wameweka kambi visiwani Zanzibar walirejea dar es Salaam jana kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya mchezo huyo muhimu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live