Sat, 30 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya KVZ ya Zanzibar imekuwa ya kwanza kutikisa nyavu za uwanja wa New Amaan Complex tangu uzinduliwe Desemba 27 licha ya kufanyika michezo mitatu bila timu yoyote kufunga bao.
Mchezaji Akram Mhina amefunga mabao yote mawili klabu yake ilipokutana na Jamhuri katika mchezo wa michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea Zanzibar.
Timu zilizocheza kwenye uwanja huo bila kufunga goli ni Zanzibar Heroes dhidi ya Kilimanjaro Stars, Azam ikiivaa Mlandege na Chipukizi ilipomenyana na Vital’O.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live