Thu, 30 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa wekundu wa Msimbazi, Simba SC, Ibrahi Ajib Migomba amejiunga na Azam FC kwa mkataba wa mwaka mmoja.
Ajibu amejiunga na Azam akitokea Simba ambako amedumu kwa misimu miwili, lakini alishindwa kujihakikishia nafasi katika kikosi cha kwanza kwa vipindi tofauti.
Ajibu mwenye umri wa miaka 25, amewahi kuzichezea Simba na Yanga kwa nyakati tofauti.
Simba SC na Ajibu waliafikiana makubaliano ya pande mbili na kusitisha mkataba wake na masaa machache akajiunga na Azam FC.
Tazama Picha zaidi akitambulishwa hapa chini;
Chanzo: www.tanzaniaweb.live