Sun, 7 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Coastal Union imethibitisha kuachana na nyota wake watatu ambao ni Haji Ugando Crispin Ngushi Na Ibrahimu Ajibu.
“Mlikuwa sehemu muhimu sana ya kikosi chetu, kujitoa kwenu kuipambania timu, hamasa ndani ya kikosi na uzoefu wenu vimekuwa msaada mkubwa ndani ya klabu yetu” imesema taarifa ya klabu hiyo.
“Hatuwezi kujivunia mafanikio tuliyoyapata bila kukumbuka mchango wenu wala hatuwezi kusahau jasho na damu mliyovuja, we ‘will miss you heroes,thank you legends,see you next time.’”
Chanzo: www.tanzaniaweb.live