Tue, 21 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Golikipa wa timu ya taifa ya Tanzania Aishi Salum Manula akizungumza mbele ya vyombo vya habari jana Novemba 20, 2023 amesema kuelekea mchezo wa kesho kati ya Taifa stars dhidi ya Morocco amekiri ugumu wa mechi hiyo.
Hiyo amesema ni kutokana na ubora wa Morocco lakini wao kama wachezaji wamejipanga na wanaitaka mechi hiyo kwani siku zote wachezaji wakubwa huzitaka mechi kubwa na hii ya leo ni mechi kubwa.
Mechi itapigwa leo usiku majira ya saa nne usiku katika Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live