Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ahmed ataja sababu ya kuachana na Zoran

Ahmed Na Zoran Ahmed ataja sababu ya kuachana na Zoran

Fri, 16 Sep 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Msemaji wa Simba Ahmed Ally amesema miongoni mwa sababu ambazo ziliwafanya wasikie hatua ya kuachana na aliyekuwa Kocha wao Mkuu Zoran Maki ni kuwakataa baadhi ya wachezaji.

Ahmed ameyasema hayo Septemba 16, 2022 alipokuwa akifanya mahojiano na Wasafi TV akielezea maandalizi yao ya mchezo dhidi ya Nyasa Big Bullets ya Malawi ambapo alipoulizwa kuhusu sababu ya kuachana na Zoran ndipo aliposema sababu hiyo.

“Hiyo ya kuwakataa baadhi ya wachezaji ni miongoni mwa sababu ambayo ilitufanya tuachane na Zoran lakini kwa ujumla tulifikia mahali tukaona hatuwezi kwenda pamoja na Zoran, na yeye akaona hawezi kufanya kazi na Simba,” alisema Ahmed.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live