Tue, 6 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya Jana Yanga kualikwa Ikulu na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kwa ajili ya chakula cha jioni ikiwa ni kama kupongezwa baada kufika Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika na kuishia kukamata nafasi ya pili.
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally ambe nae alikuwepo ikulu jana Juni 5, ameandika ujumbe katika Mtandao wake wa Kijamii wa Instagram ikiwa ni kama kijembe kwa watani zao Yanga.
Ahmed ameandika;
"Nimetoka Ikulu
Wenzetu leo wamepeleka Medali za kukosa kombe, Sisi Insha Allah sisi tutapeleka kombe Ikulu"
Chanzo: www.tanzaniaweb.live