Tue, 6 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Afisa Habari wa Simba SC, Ahmed Ally amesema klabu yao imetengeneza ubora kwa wachezaji wake na ndio maana watu wamekuwa wakiwafananisha wachezaji wao na wachezaji wa Simba.
"Simba tumeset standard za ubora, mchezaji akicheza vizuri kwenye timu zao utasikia yule ni kiungo bora kuliko Chama au yule anajua kufunga kuliko Phiri mara yule ni zaidi ya Manula.
Kwao ili mchezaji awe bora ni lazima afanane na mchezaji wa Simba Wakati sisi tunawaza kumfananisha Manula na Mohammed El Shanawy au Denis Onyango wao wanafafanisha makipa wao na Manula"
Chanzo: www.tanzaniaweb.live