Tue, 19 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally ameweka wazi kuwa ni kweli kipa wao Ayoub Lakred aliruhusu bao jepesi na la kizembe lililoigharimu timu yao dhidi ya Power Dynamos lakini amesisitiza kuwa hilo haliondoi ukubwa wa nyanda huyo na wao wataendelea kumpa nafasi zaidi kulidhihirisha hilo.
Ahmed ameongeza kuwa wachezaji bora huwa wanafanya makosa ya aina hiyo lakini haiwaondolei ukubwa wao.
Simba ilimaliza mchezo huo kwa sare ya magoli 2-2 na mchezo wa marudiano utapigwa Oktoba 1.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live