Wakati leo Bunge likiwa linatarajia kusoma Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Tume Huru ya Uchaguzi, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally na Msemaji wa Klabu ya Yanga, Ally Kamwe wamekutana Bungeni kwa mara ya kwanza baada ya Derby ya Kariakoo.
Wakati leo Bunge likiwa linatarajia kusoma Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Tume Huru ya Uchaguzi, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally na Msemaji wa Klabu ya Yanga, Ally Kamwe wamekutana Bungeni kwa mara ya kwanza baada ya Derby ya Kariakoo. Wawili hao wamekutana katika viwanja vya Bunge kuhudhuria mkutano unaondelea mjini Dodoma, ambapo itasomwa miswada ya Serikali ikiwemo Muswada wa Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa mwaka 2023, Muswada wa Sheria ya Tume ya Uchaguzi wa mwaka 2023 na Muswada wa Sheria wa Marekebisho ya Mabadiliko ya Sheria za Vyama vya Siasa wa mwaka 2023.