Tue, 14 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji wa Timu ya Taifa ya Argentina na Barcelona, Sergio Kun Aguero atatangaza mustakabali wake katika soka siku ya kesho Disemba 15, katika Mkutano na Waandishi wa Habari.
Katika Mkutano huo Aguero ataambatana na Rais wa Klabu ya Barcelona, Laporta pamoja na wachezaji wenzake wa Kikosi cha Barcelona.
Taarifa za awali zinadai kuwa Aguero anatarajiwa kutangaza kustaafu Soka la ushindani kutokana na matatizo ya moyo yanayomkabili.
Aguero amejiunga na Barcelona dirisha la usajili lililopita baada ya kumaliza mkataba wake na Man City.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live