Sat, 3 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Afya ya Gwiji wa soka duniani Edson Erantes Dos Nascimento, Pele, inatajwa kuwa katika hali mbaya na hakuna matibabu yoyote ya mionzi ambayo yanaweza kumfanya awe sawa.
Baadhi ya vyomo vya habari vimeripoti kuwa amewekwa kwenye uangalizi maalum wa kupunguza maumivu na asipate changamoto ya pumzi kwa wakati huu ila hakuna tiba ambayo inaweza kutatua changamoto yake.
Pele anabaki kuwa mchezaji pekee kubeba Kombe la Dunia mara tatu ambapo amefanya hivyo akiwa na Brazil 1958, 1962, 1970.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live