Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Adolf Mtasigwa kutua Yanga

Mtasigwazaz Adolf Mtasigwa kutua Yanga

Sun, 9 Jun 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Siku chache baada ya sintofahamu ya kukosa saini ya kiungo, Yusuph Kagoma, mabosi wa Yanga wapo kwenye mchakato wa kuibomoa Azam FC kwa kumnasa kiungo fundi, Adolf Mtasingwa aliyebakiza mkataba wa miezi sita kuitumikia timu hiyo.

Mwanaspoti linafahamu, Yanga kwa usiri mkubwa imeanza mazungumzo na kiungo huyo aliyekuzwa timu ya Vijana ya Azam aliyeng’ara katika mechi ya Fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Yanga akichuana vikali na mastaa wa Yanga, Khalid Aucho, Mudathir Yahya na baada Jonas Mkude.

Taarifa zaidi zinasema Yanga imepata mzuka wa kumbeba kiungo huyo wanayeona anaweza kuwa mbadala sahihi wa Aucho, huku ikielezwa amegoma kuongeza mkataba mpya na wana lambalamba hao.

Nyota huyo aliyewahi kukichezea kikosi hicho akiwa akademi amerejea nchini baada ya mkataba wake kumalizika na uongozi wa Azam FC kumpa mkataba wa mwaka mmoja.

Chanzo cha kuaminika kutoka kwa rafiki wa karibu wa mchezaji huyo kimeliambia Mwanaspoti, Mtasigwa amechomoa kusalia Chamazi baada ya kupata ofa kadhaa ikiwamo ya Yanga, wakati mkataba na klabu hiyo ukibakiza miezi michache kabla ya kumalizika.

“Mtasingwa kabakiza miezi sita tu alisaini mwaka mmoja kuitumikia Azam, kwani hawakuwa na imani naye kutokana na kutokumfuatilia akiwaVolsungur IF ya Iceland baada ya kuwavutia sasa wanapambana kumwongeza mkataba mpya, lakini naye hajaonyesha nia ya kubaki kutokana na kupokea ofa kubwa,” kilisema chanzo hicho na kuongeza;

“Amepokea ofa kutoka Yanga na wameonyesha nia ya kumpa dau kubwa ambalo limemchanganya nyota huyo wa Kitanzania ambaye anakipiga kunako Azam FC. "

Chanzo: www.tanzaniaweb.live