Baada ya mabao mawili aliyofunga dhidi ya Juventus, Ademola Lookman sasa amekuwa ni mmoja kati ya wachezaji wawili pekee waliofunga 10+ msimu huu katika Serie A.
Victor Osimhen / Nigeria (mabao 13)
Ademola Lookman / Nigeria (mabao 11)
Ademola Lookman pia sasa ni mmoja kati ya Wachezaji wawili pekee waliohusika katika mabao mengi zaidi msimu katika Serie A.
Victor Osimhen / Nigeria (16)
Ademola Lookman / Nigeria (14)
Ademola Lookman katika Serie A msimu huu hadi sasa
michezo 18
dakika 1092
mabao 11
pasi za mabao 3
amehusika katika mabao 14
Ana wastani wa kufunga bao kila baada ya dakika 99, ana wastani wa kuhusika katika bao kila baada ya dakika 78.
Ademola Lookman pia amekuwa mchezaji wa nne wa Atalanta kufunga mabao 10+ baada michezo 18 katika msimu wake wa kwanza wa Serie A, baada ya Jørgen Sørensen (1949-50), Karl Aage Hansen (1949-50) na Poul Rasmussen (1952-53).