Sun, 10 Apr 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Dakika 45 za Kipindi cha Kwanza zinakamilika katika Dimba la Benjamini Mkapa si kwa wenyeji Yanga wala Geita Gold aliefanikiwa kupata goli mchezo wa Robo Fainali Kombe la Shirikisho la Azam Sports.
Yanga wamefanikiwa kufanya majaribio kadhaa katika kusaka goli lakini kukosa umakini kumewagharimu kutoweza kupata goli.
Mabeki wazoefu wa Geita Gold, Kelvin Yondani na Juma Nyoso umekuwa nguzo katika safu ya ulinzi ya Geita Gold.
Kipindi cha pili pengine walimu watakuja na mbinu mbadala kila mmoja kuona anafaniukiwa kuibuka na ushindi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live