Wed, 16 Feb 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ni dakika 45 chungu kwa Maafande wa Ruvu Shooting, baada ya kushuhudia wakiruhusu magoli matano kipindi cha kwanza kutoka kwa Simba SC.
Mchezo huo wa hatua ya 16 Bora ya Kombe la Azam Sports Federation, umemshuhudia nahodha wa Simba John Bocco akifunga magoli mawili na kumaliza ukame wa mabao uliokuwa ukimsakama.
Kiungo Clatous Chama amefunga magoli mawili huku mlinzi wa Ruvu Masinda akijifunga goli la tano.
Je, Kocha Boniface Mkwasa ataweza kugeuza ubao katika dakika 45 za Kipindi cha Pili?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live