Sat, 14 May 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Dakika 90 zimekamilika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa ambako kulikua na Mtannange wa Robo Fainali Kombe la Azam kati ya Simba SC dhidi ya Pamba.
Mchezo huo umemalizika kwa Simba ambao ndi mabingwa watetezi kuibuka na ushindi mnono wa magoli 4-0.
Magoli ya Simba katika mchezo wa leo yamefungwa na Winga Peter Banda, Kubu Dennis na Yusph Mhilu aliefunga mabao mawili.
Ushindi huo unawavusha Simba mpaka hatua ya nusu Fainali ambako anakwenda kukutana na Mtani wake wa Jadi Timu ya Yanga.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live