Simba usiku wa jana walikuwa wenyeji wa Dar City katika mchezo wa Kombe la Azam Sports Federation hatua ya 32 Bora.
Katika mchezo huo Simba waliokuwa hawajapata ushindi katika mechi zake tatu zilizopita waliibuka na ushindi wa magoli 6-0.
Magoli ya Simba katika yalifungwa na Meddie Kagere aliefunga magoli mawili(2), Clatous Chama, Mugalu, Bwalya na Beki Paschal Wawa.
Ushindi huo umewavusha Mabingwa hao watetezi kwa Raundi ya Tano ya michuano hiyo (Hatua ya 16 Bora)
Tazama hapa chini Magoli yote katika mchezo huo,
???? Magoli 6️⃣ ya ushindi dhidi ya Dar City katika #ASFC #NguvuMoja pic.twitter.com/YbBBZlrq1d
— Simba Sports Club (@SimbaSCTanzania) January 30, 2022