Fri, 3 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Dakika 45 za kipindi cha kwanza zinakamilika katika Uwanja wa Azam Complex mchezo wa hatua ya 16 Bora kati ya Yanga dhidi ya Tz Prisons.
Yanga wametawala eneo kubwa la mchezo huku wakipiga mashuti 8 yaliyolenga lango na kutawala mchezo kwa zaidi ya Asilimia 70.
Kipindi cha Pili Prison watakuwa na kazi kubwa ya kufanya huku wakiwa pungufu baada ya mchezaji wao Abraham Ibrahim kuoneshwa kadi nyekundu kwa kumchezea madhambi Tuisila Kisinda, lakini awali alianza kumchezea madhambi Jesus Moloko.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live