Rivers United ya Nigeria inayoanza na Yanga kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, itashiriki michuano mifupi nchini Benin ambayo AS Vita ya DR Congo ni moja ya washiriki.
Rivers United wamethibitisha kushiriki michuano hiyo ya Chalenji ya Afrika Magharibi, na wataitumia kuipima timu kujiandaa na msimu mpya.
Michuano hiyo imepangwa kuanza leo Alhamisi mpaka Jumatano ijayo nchini Benin, huku timu shiriki ni Hearts of Oak (Ghana),Union Sportive de la Gendarmerie Nationale (Niger), Horoya Athletic Club (Guinea), Arta Solar 7 (Djibouti), Loto-Popo FC (Benin), Vita Club (Congo) na AS Sonabel FC (Burkina Faso). Zipo nyingine ni Les Buffles (Benin) na Rivers United FC (Nigeria).