Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, amesema Shindano la Africa Footbal League (AFL) la mwaka huu ndio lina hadhi kubwa kuliko litakalofanyika misimu inayofata.
Ahmed ameyasema hayo leo Oktoba 17, 2023 alipokuwa akifanya hamasa za kuelekea kwenye mchezo wa ufunguzi dhidi ya Al Ahly ya Misri utakaochezwa Ijumaa hii Oktoba 2023 katika dimba la Benjamini Mkapa jijini Dar.
"Maandalizi haya babkubwa yanayofanyika yanatuhitaji kwenda uwanjani. Hakuna Mwanasimba anatakiwa kubaki nyumbani, hiyo siku ni kwenda uwanjani. Historia hiyo itabaki kwa vizazi na vizazi."
"Lazima tuambiane ukweli AFL ya safari hii imeshirikisha timu nane bora na Mnyama yupo kati ya timu hizo bora, AFL zijazo zitakusanya kila mtu ambayo haitakuwa na thamani sawa na hii ya kwanza."- Ahmed Ally.