Tue, 5 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mlinda mlango wa timu ya taifa Nigeria ‘Super Eagles’ Stanley Nwabali (27) ameanza kutamaniwa katika ligi za Saudia Arabia na Uingereza.
Nwabali amefanya vyema katika Mashindano ya Mataifa Afrika (AFCON) yaliyofanyika nchini Ivory Coast na taifa hilo likabakiza kombe hilo nyumbani kwa kuifunga Nigeria ya Nwabali.
Kipa huyo anayekipiga Chippa United ya Afrika Kusini huenda akaondoka klabuni hapo itakapofika usajili wa majira ya joto baadae.
Klabu ya Queens Park Rangers ya England ( Daraja la Pili ) na El Ittifaq ya Saudi Arabia zipo mstari wa mbele kuiwania saini ya kipa huyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live