Mashindano ya kombe la Mataifa Afrika 2023 (AFCON2023) yanaendelea kutimua vumbi leo Januari 27, 2024 kwa mechi mbili za hatua ya mtoano 16 bora (playoffs) za kusaka tiketi ya robo fainali.
Mtanange wa mapema saa 2:00 usiku utaikutanisha miamba kutoka ukanda wa COSAFA, Angola dhidi ya Namibia katika dimba la de La Paix mjini Bouaké.
Mchezo mwingine utawakutanisha Mabingwa wa AFCON 2013 Nigeria dhidi ya Mabingwa wa 2017, Cameroon katika dimba la Felix Houphouet-Boigny majira ya saa 5:00 usiku.
Angola vs Namibia
Uwanja: Stade de la Paix
Muda: Saa 2:00 usiku
Nigeria vs Cameroon
Uwanja: Stade Felix Houphouet-Boigny
Muda: Saa 5:00 USIKU