Sat, 4 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya AC Milan imetangaza kuwa haikuwa inafahamu chochote kuhusu uraibu wa kucheza kamari wa kiungo wake wa zamani, Sandro Tonali kabla ya kumuuza kwenda Newcastle United ya England.
"Tulipata taarifa ya kuhusu uraibu wa Tonali wa kucheza kamari kupitia ripoti za vyombo vya habari, tunachojua ni kile tunachosoma tu. Hatujui kitu kingine chochoteā.
Tonali (23) alifungiwa miezi 10 kujihusisha na masuala ya soka kwa kukiuka sheria za michezo ya kubashiri za Italia ambapo atatumia miezi 8 kushiriki katika mpango wa kutibu uraibu wake wa kucheza kamari.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live