Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

2021 Mwaka Mgumu kwa Sergio Ramos

Ramos Sergiooo Sergio Ramos aoneshwa kadi nyekundu

Sun, 26 Dec 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwaka 2021 hakika ni mwaka ambao beki kisiki Sergio Ramos hatousahau kutoka ulivyoanza mpaka unavyoisha kwa mambo yaliyomtokea.

Mwezi Januari ilionekana kama kuwa na neema baada ya Real Madrid kuonyesha dalili za kumpa makataba mpya na kwenda na timu ya taifa kwenye michuano ya Ulaya lakini mambo ghafla ya libadilika na majanga yakaanza kumuandama.

Januari alipata tatizo la tumbo hali iliyopelekea kukosa mechi za Real Madrid na katikati ya mwezi alipata tatizo lingine la mguu katika mchezo waliopoteza katika michuano ya Supercopa de Espana.

Mwezi wa pili tatizo lake la mguu lilihitaji kufanyiwa upasuaji na Februari 6 alifanyiw upasuaji hali iliyopelekea kukaa nje ya dimba kwa wiki sita mpaka nane.

Machi aliga kuichezea timu ya taifa wakati kampeni ya michezo ya kufuzu kombe la Dunia ilipoanza baada ya Luiz Enrique kutokuwa na mipango na beki huyo.

Mwezi wa Nne Ramos hakucheza hata dakika moja kwa Madrid kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2013 Mei.

Mwezi Mei Ramos alisafiri na kiksi cha Real Madrid mpaka London kuikabili Chelsea ambapo Los Blancos walitolewa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa.

Juni ndiyo ilikuwa mwisho wa Ramos kuwa sehemu ya klabu ya Real Madrid na alisema hakutaka kuondoka lakini hilo lilikuwa ni kweli hatoendelea na Real Madrid.

PSG walimsaini Sergio Ramos mwezi Julai huku akitarajia kutua Ufaransa akifuatiwa na majina makubwa kutua klabuni hapo.

Mwezi wa 8,9 na 10 Ramos hakuwa kuichezea klabu ya Paris Saint-Germain wakati Novemba 9 alirejea mazoezini lakini hakuweza kucheza mpaka tarehe 28 alipocheza dhidi ya Saint-Etienne lakini badaye alirejea kwenye orodha ya majeruhi.

Mwezi Disemba Ramos alimaliza mwaka wake mbaya kwa kutolewa nje kwa kadi nyekundu. Sio wewe pekee unayesubiri mwaka 2022 kwa hamu kubwa bali hata Ramos naye anashuku kubwa ya kumalizana na mwaka 2021 sababu ya magumu aliyopitia.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live