Ndege hiyo ya kampuni ya Auric air yenye namba 5H-AAM iliyokuwa inaendeshwa na Nelson Mabeyo mtoto wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Tanzania, Venance Mabeyo imepata imeanguka leo Jumatatu asubuhi Septemba 23, 2019.
Katika ndege hiyo kulikuwa na Nelson na Nelson Orutu ambaye inadaiwa ni rubani mwanafunzi lakini si wa kampuni hiyo ambo wote kwa pamoja walifariki ndani ya ndege hiyo iliyoanguka muda mfupi baada ya kuruka kwenda kuwabeba wageni hao waliokuwa Grumeti Kirawira.
SOMA ZAIDI: Mtoto wa mkuu wa majeshi Tanzania afariki ajali ya ndege
Msimamizi wa kampuni hiyo kwa Serengeti, Peter Kimaro ameiambia Mwananchi kuwa wamebadilisha safari za ndege zao mbili na kwenda kuwachukua wote na kuwapeleka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
"Wageni hao walikuwa wa kampuni ya And beyond Tanzania na sisi tulikodiwa kuwasafirisha, baada ya tukio tukachukua hatua ya haraka maana wale walikuwa na ratiba yao," amesema.
Habari zinazohusiana na hii
- Ndege yaanguka hifadhi ya Serengeti Tanzania, yaua wawili
- Mtoto wa mkuu wa majeshi Tanzania afariki ajali ya ndege
- Helikopta ya JWTZ yatua Serengeti kuchukua mwili wa mtoto wa Mabeyo
>Helikopta ya JWTZ yatua Serengeti kuchukua mwili wa mtoto wa Mabeyo