Dini

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wanafunzi wataka wenzao wanaokwenda na bangi shule kudhibitiwa

67945 Pic+wanafunzi

Tue, 23 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Unguja. Baadhi ya wanafunzi wa Shule  ya Sekondari Fuoni Mkoa wa Mjini Magharibi kisiwani Zanzibar wameukata uongozi wa shule hiyo kuwadhibiti wenzao wanaokwenda shule wakiwa na dawa za kulevya aina ya bangi na kuzificha chooni.

Wametoa kauli hiyo leo Jumanne Julai 23, 2019 katika mkutano ulioandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wakawake (Tamwa) Zanzibar  na dawati la jinsia la Jeshi la Polisi.

Mmoja wa wanafunzi , Abdalla Majid amesema mara kadhaa amewashuhudia wenzake wakivuta bangi chooni na nyingine kuzificha, kwamba hali hiyo inasababisha baadhi yao kuishia chooni badala ya kwenda darasani.

Summaya Kheri amesema baadhi yao huwa na nguo katika mabegi  jambo linaloashiria kuwa huvua sare za shule na kuvaa nguo hizo.

Kuhusu udhalilishaji kwa wanafunzi,  Saida Kheri ameuomba uongozi wa shule hiyo kujenga uzio, kwamba kukosekana kwake ndio chanzo cha kuibuka kwa udhalilishaji.

Akijibu kuhusu uzio, sheha wa shehia ya Fuoni Uwandani,  Juma Mussa Juma amesema jitihada mbalimbali zimeanza kufanywa kujenga uzio huo.

Pia Soma

Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Haji Nassor amesema baadhi ya wanafunzi kutoingia darasani  huku wenzao wakiendelea na masomo kunarudisha nyuma jitihada za walimu kufundisha, kushusha ufaulu katika mitihani ya mwisho.

Chanzo: mwananchi.co.tz