Menu ›
Dini
Thu, 23 Mar 2023
Chanzo: Bbc
Waislamu wameanza kufunga mwezi mtukufu wa Ramadhan siku ya Alhamisi duniani kote baada ya mwezi kuandama majira ya jioni siku ya Jumatano.
Nchini Kenya, Naibu Kadhi Mkuu Sheikh Sukyan Hasan nchini Kenya alitangaza kuonekana kwa mwezi katika baadhi ya Kaunti za Mandera, Wajir na Tana River siku ya Jumatano Jioni.
Ramadhan ambao ni mwezi wa tisa wa kalenda ya Kiislamu, unachukuliwa kuwa mtakatifu zaidi na Waislamu.
Waumini wametakiwa kuungana wanapoanza saumu yao na kuepuka jambo lolote litakaloingilia mfungo wao.
Chanzo: Bbc