Menu ›
Dini
Sun, 9 Sep 2018
Chanzo: mwananchi.co.tz
Mwanachi. Mwili wa muimba kwaya ya Vijana ya Kanisa la AICT Chang'ombe (CVC), Mariam Charles (22), umewasili kanisani hapo kwa ajili ya ibada ya mazishi.
Vilio na simanzi vilitawala kanisani hapo wakati mwili huo ukiwasili na kupokelewa na wanakwaya wenzake.
Mariam anadaiwa kuuawa kwa kunyongwa na mwili wake ulikutwa usiku wa kuamkia Septemba 5 katika nyumba ya kulala wageni ya 'East London’ iliyopo Buza anakodaiwa alikuwa na mchumba wake.
Soma Zaidi:
Sakata la mwanakwaya kufia gesti, ndugu watumiwa meseji za vitisho
Chanzo: mwananchi.co.tz