Dini

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

VIDEO: Mchungaji Getrude Rwakatare aeleza maana ya upepo wa Kisulisuli

VIDEO: Mchungaji Getrude Rwakatare aeleza maana ya upepo wa Kisulisuli

Mon, 21 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Kama ni mfuatiliaji wa mitandao ya kijamii nchini Tanzania lazima utakuwa umekumbana na neno ‘upepo wa kisulisuli’.

Neno hilo limekuwa maarufu na sasa umekuwa kama utani, kwani wapo wanahusisha mambo yao kwenda sawa kama kasi ya upepo wa kisulusuli.

Neno hilo limekuwa maarufu baada ya video iliyosambaa mitandaoni kumuonyesha mchungaji kiongozi wa kanisa la Mlima wa Moto, Dk Getrude Rwakatare akiwaita madhabahuni wanawake na wasichana ambao hawajaolewa ili awafanyie maombi na watawapata wenza wao kwa “upepo wa kisulisuli.”

Neno Kisulisuli lipo katika Biblia takatifu katika kitabu cha Hesabu likiwa na maana ya muujiza.

Maana hiyo ndiyo iliyomfanya mchungaji Rwakatare kulitumia kuwaombea wanaohitaji kupata wenza.

 “Nimefurahi maana nimeona ujumbe umefika kwenye jamii na umewagusa wanawake na wanaume kwa kuwa tatizo hilo lipo na pande zote zina uhitaji.”

Pia Soma

Advertisement
“Nasikia inavyojadiliwa na wengine wanatengeneza vichekesho nimeona moja inasema ‘Baba amejikuta kwenye chumba cha msichana wa kazi baada ya kukumbana na upepo wa kisulisuli’. Mimi nataka wale wanaotaka kuoa na kuolewa,” amesema mchungaji huyo.

Chanzo: mwananchi.co.tz