Askofu wa Jimbo la Rulenge Ngara Mhashamu Severine Niwemugizi amesema kuwa kanisa katoliki litaendelea kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya Sita katika kuboresha kiwango Cha taaluma kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.
Mhashamu Baba Askofu Severine Niwemugizi, amebainisha hayo wakati wa maadhimisho ya wiki ya elimu iliyofanyika katika shule ya sekondari Severine wilayani Biharamulo mkoani Kager akisisitiza ufundishaji wa nadhalia na vitendo ili kumjenga mwanafunzi katika misingi ya Uongozi bora
Askofu huyo amesema kuwa lengo la kuunga mkono juhudi za Serikali ni kwa sababu Kanisa hilo linapenda kuona taifa likiwa wataalamu wenye sifa zinazoendana na soko la ajira kimataifa na kikanda hasa ukanda wa Afrika wa Mshariki.