Sheikh wa mkoa wa Tabora Ibrahim Mavumbi, amesema upo umuhimu mkubwa wa kuwajengea watoto misingi imara ya dini itayowaongoza kuishi katika maadili mazuri na kuepukana na vitendo vya uhalifu wa kutumia nguvu na silaha ambavyo vimekuwa vikifanywa na vijana wadogo.
Sheikh Mavumbi ametoa kauli hiyo alipohudhuria mashindano ya Qu,rani ambayo yameandaliwa na taasisi ya kiislamu ya Al tijarah al rabiha charitable foundation kupitia chuo chake ya Maahad Oman Islamic kilichopo eneo la Ibologero, wilayani Igunga mkoani Tabora .
Amesema kwa sasa kumekuwa na anguko kubwa la maadili kwa watoto hatua ambayo imekuwa ikisababisha wengi kujiingiza katika matukio ya uhalifu.