Dini

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rombo hakujatulia, Kanisa Katoliki lataja mkakati wa kuwanusuru vijana

64853 Rombo+pic

Sat, 29 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Rombo. Ulevi uliopindukia hasa kwa vijana wenye umri kuanzia miaka 18 na kuendelea wa kujihusisha na unywaji pombe haramu ya gongo wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro umekua ni chukizo kwa jamii na baadhi ya viongozi wa dini.

Kutokana na hali hiyo, viongozi wa Kanisa Katoliki Rombo wameendelea kupigilia msumari watengenezaji wa pombe hizo wakisema endapo hawataacha kutengeneza   watatengwa na kanisa pamoja na waumini wa dini hiyo kwani pombe hizo zinaharibu nguvu kazi ya vijana wengi

Kauli ya kutengwa  kwa watengenezaji gongo imesemwa juzi Alhamisi Juni 27, 2019 na Mkuu wa vikarieti ya Vunjo, Padre Valerian Msafiri  wakati wa adhimisho la  misa Takatifu ya Jubilee ya miaka 50 ya Halmashauri ya Walei iliyofanyika katika  Parokia ya Mtakatifu Yohane Mbatizaji.

“Leo tunasherekea sikukuu ya kuzaliwa kwake Yohana Mbatizaji, alijitenga na maovu, alikataa dhambi, nyie mnafanya nini kwa nini msiwatenge hao watengenezaji gongo? mnasubiri nini watengeni, mkifanya hivyo mtafanana na Yohane Mbatizaji  na wilaya yenu  itakua na Mwanga,” alisema Padre Msafiri.

Awali, akisoma taarifa ya Parokia hiyo, Katibu wa Parokia, Eleuter  Massawe amesema changamoto kubwa katika wilaya hiyo ni ulevi uliopindukia hasa vijana  ambapo wengi wao wamekua wakinywa  gongo  hali ambayo inawafanya washindwe kufanya kazi ya kuzalisha.

“Changamoto kubwa iliyopo katika wilaya yetu ni kukithiri kwa unywaji wa gongo hasa kwa vijana, wengi wao wamekua wakinywa pombe haramu ya gongo na pombe nyingine ambazo hazina viwango jambo ambalo linawaangamiza vijana wengi,” alisema Massawe.

Pia Soma

Mmoja wa wakazi wa Rombo, Agripina Tesha alisema kanisa kuwatenga wanywa gongo itasaidia sana kwani itakua ni fundisho kubwa hivyo adhabu hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza utengenezaji na unywaji wa gongo.

“Kutengwa na kanisa ni adhabu kubwa sana katika dini yetu, hivyo uamuzi huo ukitekelezeka watu hawa huenda wakapunguza kutengeneza pombe hizo, kanisa linafanya vizuri sana ili kuokoa kizazi kijacho, maana vijana wetu wengi wameharibiwa na pombe hata kufanya kazi za kuzalisha hawawezi tena,” alisema Tesha.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz