Dar es Salaam. Rais wa Baraza la Maaskofu (TEC), Mhashamu Gervas Nyaisonga amewataka waamini kupokea msiba uliolikumba Kanisa Katoliki baada ya maaskofu wastaafu wawili kufariki dunia juzi na usiku wa kuamkia jana.
Maaskofu hao ni Gabriel Mmole aliyetumikia jimbo la Mtwara na ambaye alifariki Mei 15, na walitumikia majimbo ya Mtwara na Emmanuel Mapunda aliyetumikia jimbo la Mbinga.
Amesema huo ni msiba mkubwa na mzito, lakini waamini waupokee kwa kuwa mapenzi ya Mungu yametimizwa.
Nyaisonga, ambaye pia ni askofu wa Jimbo Kuu la Mbeya, alitoa kauli hiyo jana alipozungumza na Mwananchi, huku akiwataka Wakatoliki na wananchi kwa ujumla nchini, kutoshtushwa na vifo vya maaskofu hao kwa sababu ni vifo vyema.
“Watu wasishtuke sana. Hawa waliofariki dunia ni maaskofu wetu waliotumikia na wana umri wa zaidi ya miaka 80,” alisema.
“Sasa unajua unapokuwa mzee mwili unakuwa dhaifu kiasi. Wasishtuke ni vifo vyema na vimewakuta katika uzee na ukiwa katika hatua hii, mwili unaweza ukapata shida.”
Pia Soma
- Kodi ya zuio majanga
- Wageni waonywa mifuko ya plastiki
- Membe amjibu Rostam urais mwaka 2020
- Mkindi: Kilimo bado hakijapewa hadhi ya kuwa uti wa mgongo
Alisema Askofu Mmole aliongoza jimbo la Mtwara kwa miaka mingi, wakati Mapunda aliongoza Mtwara kwa zaidi ya miaka 25.
Kwa mujibu wa katibu mkuu wa TEC, Padri Charles Kitime maziko ya Askofu Mmole (80) yatafanyika Mei 21, mkoani Mtwara, wakati Askofu Mapunda (84) atazikwa Mei 24 wilayani Mbinga mkoani Ruvuma.