Menu ›
Dini
Tue, 5 Jan 2021
Chanzo: habarileo.co.tz
Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi ameihakikishia Jumuiya ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA) kuwa serikali itashirikiana vyema na jumuiya hiyo kwenye kujenga misingi ya dini ya kiislamu visiwani humo.
Dk Mwinyi amesema hayo alipofanya mazungumzo na viongozi wa jumuiya hiyo wakiongozwa na Kaimu Katibu wao, Sheikh Ali Abdalla Amour Ikulu ya Zanzibar.
“Nasema wazi miongoni mwa mambo makubwa yanayopaswa kupewa kipaumbele katika kujenga misingi ya dini ya Kiislamu ni umoja, amani na mshikamano” amesema Dk Mwinyi.
Chanzo: habarileo.co.tz