Dini

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nabii Mwamposa aaga waumini Dar aelekea Moshi kuitikia wito wa Polisi

94120 Mwamposaa1+pic Nabii Mwamposa aaga waumini Dar aelekea Moshi kuitikia wito wa Polisi

Mon, 3 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Kiongozi wa kanisa la Inuka Uangaze, Nabii na mtume Boniface Mwamposa amelazimika kusitisha ibada kwa ajili ya kuitikia wito wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Tanzania  kulikotokea vifo vya waamini wake.

Mwamposa ambaye huendesha ibada zake katika eneo la Tanganyika Packers, leo Jumapili Februari 2, 2020, amelazimika kufupisha ibada ya kwanza na kuanza safari ya kuelekea Moshi alikoitwa na polisi.

Kawaida ibada hiyo huisha kati ya saa saba hadi saa nane mchana, lakini leo imeisha saa 4:30.

Mwamposa akiwa ameambatana na wasaidizi wake, aliondoka katika eneo hilo la Kanisa 4:30 asubuhi hii.

Jana katika kongamano lake la kukanyaga mafuta ya upako mkoani Kilimanjaro, watu 20 walipoteza maisha wakisukumana kukanyaga mafuta hayo.

Wakati hayo yakiendelea, waumini wa nabii huyo wamemkingia kifua na kueleza suala la watu kukanyagana kwenye mikutano mikubwa ni kawaida.

Habari zinazohusiana na hii

Advertisement
 “Watu wanaongea sana ila sisi tupo pamoja naye, suala la kukanyagana sio kitu cha ajabu na yeye hana kosa ni watu wenyewe kushindwa kufuata utaratibu. Mungu atamsaidia ataungana nasi,” amesema muumini huyo aitwaye Neema Mbinga.

Chanzo: mwananchi.co.tz