Dini

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mzee wa Upako atoa neno serikali za mitaa

83650 Pic+lusekelo Mzee wa Upako atoa neno serikali za mitaa

Thu, 14 Nov 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Wakati mjadala mkubwa nchini Tanzania ukiendelea kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa baada ya baadhi ya vyama kadhaa vya upinzani kutangaza kususia uchaguzi huo kwa madai ya kuonewa kwa wagombea wao, wadau mbalimbali wametoa maoni yao kuhusu uchaguzi huo.

Moja ya watu waliotoa maoni yao ni Mchungaji wa Kanisa la GRC, Jijini Dar es Salaam, Antony Lusekelo (Mzee wa Upako) ambaye anasema wananchi wanatakiwa kupewa uhuru wa kuchagua viongozi wanaowataka kutoka kwenye vyama vya upinzani.

“Vyama vya siasa visiingiliwe, vishindane na vikubaliane na matokeo baada ya uchaguzi.

“Sisi tunaendelea kuwapatia watu elimu kwamba wawachague viongozi wasioendekeza rushwa na watakaofaa kuongoza kwenye maeneo yao,” alisema Lusekelo.

Vyama vya upinzani vikiwemo Chadema na ACT- Wazalendo wametangaza kujitoa katika uchaguzi huo baada ya kudai kuwa wagombea wao wengi wameondolewa katika uchaguzi huo kinyume na taratibu .

Chanzo: mwananchi.co.tz