Dini

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwanamke ajirusha ndani ya kaburi la Padre baada ya maiti kushushwa

Mchtt Kaburii Mwanamke ajirusha ndani ya kaburi la Padre baada ya maiti kushushwa

Thu, 23 Mar 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwanamke mmoja amewashangaza waombolezaji katika hafla ya kuaga mwili wa padre mmoja wa kanisa baada ya kujitupa kwenye kaburi la mchungaji huyo alipokuwa anazikwa.

Katika kisa hicho ambacho kimeenezwa pakubwa mitandaoni, mwanamke huyo ambaye hakujulikana alionekana anajongea kwenye kabiri la padre aliyetambuliwa kwa jina moja tu – Benerd ambalo lilikuwa limewekwa maua baada ya mwili kuteremshwa.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa eneo la tukio, mwanamke huyo alifika kwenye makaburi hayo akiwa amevalia vazi refu jeusi na nyeupe pamoja na stara.

Jeneza la Baba Bernard lilipokuwa likishushwa chini, ghafla alikimbia kuelekea kaburini na kuruka ndani. Alisikika akipiga kelele na kulia bila kujizuia kabla ya kuvutwa nje na wafanyakazi wa makaburi.

Tukio hilo lilinaswa kwenye video na kusambazwa kwenye Instagram, ambapo lilisambaa haraka haraka. Watu wengi wamekuwa wakionyesha mshtuko na kuchanganyikiwa kwa kitendo cha mwanamke huyo, huku wengine wakikisia kuwa huenda alikuwa ndugu au rafiki wa karibu wa marehemu.

Padre Bernard alikuwa mwanajumuiya aliyeheshimika sana na alikuwa amehudumu kama kasisi kwa miaka mingi. Kifo chake cha ghafla kimewaacha wengi wakiwa na huzuni, na matendo ya mwanamke huyo yameongeza tu mkanganyiko na huzuni inayozunguka kuzikwa kwake, mmoja alinukuliwa akisema.

Visa vya watu kujitupa kwenye makaburi ya wapendwa wao si vigeni kuripotiwa. Itakumbukwa mwaka 2018 mwanamke mmoja kutoka kaunti ya Nakuru aligonga vichwa vya habari baada ya kunaswa kwenye kamera akifanya kufuru ya kuruka kwenye kaburi la mume wake, kama njiqa ya kuonesha simanzi yake kutotaka kumuaga kabisa mpenzi wake.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live