Dini

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwamposa: Watu wavae barakoa wanapokuwa kanisani wasione aibu

102229 Pic+mwamposa Mwamposa: Watu wavae barakoa wanapokuwa kanisani wasione aibu

Mon, 13 Apr 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam.Kiongozi wa Kanisa la Inuka Uangaze, Mtume Boniface Mwamposa amesema watu wasione aibu kuvaa barakoa(mask) wanapokuwa kanisani hivyo wanatakiwa kuvaa ili wajilinde na ugonjwa wa corona. Mwamposa amezugumza hayo wakati wa ibada ya pasaka amesema unapovaa barakoa kanisani siyo kwamba hauna imani hivyo lazima ufuate maelekezo yaliyotolewa na Serikali jinsi ya kujikinga na ugonjwa huo. Amesema ukimuona mtu amevaa barakoa  kanisani siyo kwamba hamuamini Mungu  bali anajikinga na corona usione haya kuvaa unapokuwa kanisani au barabarani lazima mfuate masharti kama Serikali inavyosema.

"Usimjaribu Mungu wako kwa kusema eti umeokoka huwezi kufuata maelekezo ya Serikali jinsi ya kujikinga na ugonjwa wa corona  hivyo utakufa  lazima ujikinge huku ukimuomba Mungu atuepushe mfano tumeona leo kila muumini anakaa mita moja kutoka kiti kingine hivyo hivyo mnapokuwa nyumbani mnatakiwa mkae mbalimbali, kunawa mikono na kutogusana," amesema Dk Mwamposa.

Pia amesema siku ya ufufuko wa Yesu kristo kila mtu aliyekuwemo kwenye ibada hiyo watafunguliwa mambo mbali mbali ikiwemo wagonjwa watapona na watu watafunguliwa kiuchumi, kikazi na kielimu.

Chanzo: mwananchi.co.tz