Dini

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mufti wa Tanzania amzungumzia aliyechana kitabu cha dini

95008 Pic+muft Mufti wa Tanzania amzungumzia aliyechana kitabu cha dini

Mon, 10 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Korogwe. Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeir ameipongeza Serikali kwa hatua ilizozichukua dhidi ya Daniel Maleki anayedaiwa kuchana kitabu cha dini.

Jana Ijumaa Februari 7, 2020 picha za video zilizosambaa katika mitandao ya kijamii zilimuonyesha Maleki ambaye ni ofisa biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mkoa wa Morogoro akichana kitabu hicho.

Muda mfupi baada ya kusambaa kwa video hizo, alikamatwa na polisi na kufikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kilosa ambako alisomewa mashtaka na kupelekwa mahabusu baada ya polisi kuwasilisha ombi la kutaka asipewe dhamana.

Mufti ameeleza hayo leo Jumamosi Februari 8, 2020  katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu tukio hilo.

Amesema kuchanwa kwa kitabu hicho  hadharani ni kuwachokoza Waislamu  na kuvuruga amani na utulivu wa Watanzania.

“Ninaishukuru Serikali kwa hatua iliyochukua dhidi ya kijana huyu, nawaomba Waislamu kuwa watulivu, wasubiri hatua zaidi

Habari zinazohusiana na hii

Advertisement
atakazochukuliwa nikiamini kwamba hakutumwa na dhehebu lolote bali ni utashi wake binafsi,” amesema Sheikh Zuberi.

Kabla mtumishi huyo hajakamatwa wala kufikishwa mahakamani,  Waziri wa Tamisemi, Selemani Jafo baada ya kuona video hiyo aliitisha mkutano na waandishi wa habari mjini Dodoma na kumuagiza mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Kilosa kumsimamisha kazi mtumishi huyo.

Chanzo: mwananchi.co.tz