Dini

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mufti Zubeir aongoza swala ya Eid Kitaifa, mavazi kwa wanawake yagusiwa

61383 Pic+muft

Thu, 6 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Tanga.  Mufti wa Tanzania, Abubakar Zubeir ameongoza maelfu ya waumini wa dini ya Kiislamu waliojitokeza kuswali swala ya Eid el Fitr iliyoswaliwa Kitaifa katika msikitini Mkuu wa Ijumaa jijini Tanga.

Swala hiyo imeswalishwa leo Jumatano Juni 5, 2019 na Sheikh Ramadhani Mbarouk na hotuba ya Eid imetolewa na Sheikh Twahir Muhammad Al Musawa

Naibu Kadhi, Muhidin Mgoyogole amewataka Waislamu nchini kuendeleza mema waliyokuwa wakiyatenda wakati wa mwezi wa Ramadhani kwa kuwa ndivyo Uislamu unavyotaka.

Kuhusu mavazi amewaasa Waislamu hususani wanawake kuvaa nguo zenye kulinda maadili ya Uislamu ili kulinda maadili ya Uislamu.

Swala hiyo imehudhuriwa pia na Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano, January Makamba, Naibu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, Mbunge wa Tanga Mjini (CUF), Mussa Mbarouk na viongozi mbalimbali wa Serikali na siasa.

Wakizungumza kuhusu nasaha zilizotolewa na Naibu Kadhi waumini waliozungumza na Mwananchi kuhusiana na mavazi wamesema ni kweli wakati wa Ramadhani waumini walionekana kujisiri na miji ilitulia lakini kuanza leo vurugu zitaanza

Pia Soma

Yussuph Rashid amesema, “Kuna haja kwa viongozi wa dini kuishawishi Serikali ipige marufuku mavazi yasiyofaa.”

Chanzo: mwananchi.co.tz