Menu ›
Dini
Wed, 22 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir amethibitisha taarifa ya kuandama kwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
Amewaambia waandishi wa habari mkoani Dar es Salaam kuwa, kufuatia kuandama kwa Mwezi Mtukufu, Waumini wa dini ya Kiislam katika maeneo mbalimbali nchini wataanza Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan hapo kesho Machi 23, 2023.
Mufti wa Tanzania amesema Mwezi umeonekana katika maeneo mbalimbali ya Tanzania Bara, Zanzibar na Kenya.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live