Dini

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mchina mahakamani kwa tuhuma za kutaka kumpa rushwa RC Geita

30552 Mchinapic TanzaniaWeb

Fri, 7 Dec 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Geita. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Geita imemfikisha mahakamani raia wa China kwa kosa la kumshawishi mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel ili ampe rushwa ya Sh1milioni.

Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo Ijumaa Desemba 7, 2018 na Mkuu wa taasisi hiyo mkoani Geita, Thobias Ndaro inasema mshtakiwa huyo,  Cheng Li  ni mfanyabiashara wa madini.

Inaeleza kuwa alifikishwa mahakamani jana Novemba 6, 2018 mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya Hakimu Mkazi Geita,  Jovith Kato.

Akisoma mashtaka mwendesha  mashtaka wa Takukuru, Dennis Lekayo amedai mahakamani hapo kuwa Oktoba na Novemba, 2018 mshtakiwa  alimshawishi Gabriel kwa njia ya ujumbe wa simu akitaka kumpatia Sh1milioni kila mwezi.

Ilielezwa mahakamani hapo kuwa katika kuonyesha amedhamiria kutoa rushwa alituma ujumbe mwingine akimshawishi kumpelekea kiasi hicho cha fedha  na majani ya chai kutoka China.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa baada ya ujumbe huo, mkuu huyo wa mkoa alitoa taarifa Takukuru ambao waliweka mtego uliofanikisha kumkamata mshtakiwa akiwa ofisini kwa Gabriel akijiandaa kutoa rushwa ya Sh1milioni na majani hayo ya chai.

Mshtakiwa  amekwama makosa na yuko nje kwa dhamana huku kesi hiyo ikiahirishwa hadi Desemba 20, 2018.

 



Chanzo: mwananchi.co.tz