Dini

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbunge Segerea ataka uchunguzi ujenzi kituo cha polisi

67894 Segerea+pic

Tue, 23 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mbunge wa Segerea (CCM), Bonnah Kamoli ameomba kuundwa kamati kuchunguza ujenzi wa kituo cha polisi Segerea kilichoanza kujengwa mwaka 2017.

Kamoli ametoa kauli hiyo jana Jumatatu Julai 22, 2019 katika ziara yake katika  kata za jimbo hilo kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa fedha za mfuko wa jimbo, Serikali na wafadhili.

Amesema katika ujenzi huo alitoa mabati 60, naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni akitoa Sh500,000 na mkuu wa majeshi nchini (CDF), Venance Mabeyo alichangia Sh3 milioni.

"Kutokana na kusuasua kwa ujenzi wa kituo hiki cha polisi Segerea hii ni ishara za ubadhirifu, kupitia mkutano wa halmashauri kuu ya CCM kata ya Segerea natoa maelekezo ya kuundwa kwa kamati kuhusu ujenzi huu ili kubaini ukweli wake,” amesema Kamoli.

Katika hatua nyingine,  Kamoli amewasisitiza mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka  Dar es Salaam (Dawasa) kuongeza kasi ya usambazaji wa miundombinu ya maji katika kata ya Segerea.

Amewataka kuzingatia ubora wa kazi wanayoifanya  ili kufikia Oktoba, 2019 wakazi wa kata ya Kipawa waanze kupata huduma ya maji safi na salama.

Pia Soma

Mbunge huyo pia alishiriki mkutano wa halmashauri kuu ya CCM kata ya Segerea kujadili maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Chanzo: mwananchi.co.tz