Dini

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Majaliwa atamani Waislamu kuendeleza mema ya Ramadhan

61446 Wazrimkuupic

Thu, 6 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Waziri Mkuu,  kassim Majaliwa amesema utulivu na uadilifu ulioonyeshwa na Waislamu katika mwezi mtukufu wa Ramadhan unatakiwa kuendelea kila siku.

Ametoa kauli hiyo leo Jumatano Juni 5, 2019 katika maadhimisho ya baraza la Eid El Fitri lililofanyika Mkoa wa Tanga.

Majaliwa aliyekuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo amesema katika mwezi huo Waislamu wamekuwa si tu raia bora, bali wanapaswa kutolewa mfano.

“Katika kipindi cha swaumu mmeonyesha upendo, usafi na nia ya moyo hata baada ya kumalizika  kipindi cha ramadhani natamani muendelee hivyo,  niwaambie kuwa hatutakoma kuendeleza yale mazuri tuliyotenda mwezi huu, mshikamano huu na maisha yanayotufanya tuwe wamoja.”

“Ni matarajio yangu katika miezi 11 ijayo kabla ya ramadhani nyingine tutaendelea kuishi kwa amani, upendo na mshikamano kama ilivyokuwa sasa," amesema Majaliwa.

Amesema utulivu na uadilifu ulioonyeshwa ni silaha muhimu ya kupambana na maovu na uhalifu katika jamii.

Pia Soma

“Hii pia ni chachu kwa maendeleo na kudumisha haki, umoja, usawa, amani na utulivu ndani ya nchi," amesema.

Chanzo: mwananchi.co.tz