Dar es Salaam. Rais mstaafu, Jakaya Kikwete na katibu mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally ni kati ya viongozi waliopo katika ibada ya kuaga mwili wa mwanasiasa mkongwe nchini Tanzania, Balozi Ibrahim Kaduma.
Ibada ya kwanza ya kuaga mwili wa waziri huyo wa zamani wa Mambo ya Nje imeanza leo asubuhi Septemba 3, 2019 nyumbani kwake Makongo Juu jijini Dar es Salaam.
Ibada nyingine inatarajia kufanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Makongo Juu.
Yohana Kaduma amesema mwili wa baba yake utasafirishwa Alhamisi kuelekea nyumbani kwake Kibena Mkoani Njombe kwa ajili ya mazishi.
Balozi Kaduma (82) alifariki dunia akiwa nchini India alikoenda kwa ajili ya matibabu.