Dini

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Katibu TEC ataja mwarobaini kumaliza unyanyapaa

94804 Kitima+pic Katibu TEC ataja mwarobaini kumaliza unyanyapaa

Thu, 6 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) nchini Tanzania, Charles Kitima amesema mataifa mbalimbali yamefanikiwa kamaliza unyanyapaa kwa wenye maambukizi ya Virusi vya Ukimwi kwa kuhusisha suala hilo na sayansi ya dini.

Taarifa iliyotolewa leo Alhamisi Februari 6, 2020 na Baraza la Watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (Nacopha), imeeleza kuwa Kitima ametoa kauli hiyo leo katika mkutano na wadau mbalimbali uliowahusisha viongozi wa dini.

Katika mkutano huo wamejadiliana namna watakavyotekeleza mpango mkakati wa kupunguza unyanyapaa.

Mpango huo unatekelezwa na Nacopha, wakishirikiana  na Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID).

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mkutano huo uliwajengea uelewa viongozi mbalimbali wa dini, wadau na taasisi mbalimbali zinazojishughulisha na masuala ya Ukimwi.

Akichangia katika mkutano huo, Kitima amesema  sayansi na dini  vinakwenda pamoja  na kwamba viongozi hao wa kiroho  wanaaminika kwa sababu wanaonekana walinzi wa uhai unaohusishwa na Mungu.

Pia Soma

Advertisement
Kitima amesema  licha ya mataifa hayo kuwa na uwezo mkubwa kisayansi na kiteknolojia, bado  dini ina nafasi kubwa  katika mapambano dhidi ya unyanyapaa kufanikiwa.

“Ndiyo maana kiongozi wa dini akisema nikikuweka mkono utapona, watu watakuja na wataacha kwenda kupima sambamba na kuacha kunywa dawa. Yote hii kwa sababu sayansi haijaweza kupenya na teknolojia,” amesema Kitima.

Amesema baadhi yao wamesoma kwenye elimu ya chini na uwezo wao mdogo huku akitolea mfano Taifa la Marekani ambalo raia wake ni wagumu kudanganywa, kwamba huwezi ukawaambia waombewe bila kupima kwanza.

Katibu mkuu Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata), Alhaj Nuhu  Mruma ameungana na  Kitima  na viongozi wengine  waliochangia katika mkutano huo akisema afya ya waumini wa dini mbalimbali ni muhimu kama  Serikali unavyojenga uchumi wa nchi.

Msimamizi wa mradi  ya USAID ,  Gray  Saga amesema changamoto iliyopo ni  namna gani ya kushirikiana  viongozi   wa dini na mashirika akisema  mwanzoni mchakato huu ulikuwepo lakini  kipindi cha siku za hivi karibuni umekuwa ukisuasua.

Meneja wa uhamasishaji wa miradi ya jamii ya Nacopha,  Mathew Kawogo aliwaeleza washiriki  hali ya Ukimwi na unyanyapaa pamoja na malengo na vipaumbele kuhusisha taasisi na viongozi wa dini.

Chanzo: mwananchi.co.tz