Dini

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kardinali Pengo ang’atuka rasmi, Askofu Ruwa’ichi amrithi

71662 Pengo+pic

Fri, 16 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Papa Francisko ameridhia ombi la Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam nchini Tanzania, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo la kutaka kung’atuka madarakani.

Ombi la Kardinali Pengo mwenye miaka 75 la kustaafu majukumu ya kuliongoza jimbo hilo yameridhiwa leo Alhamisi Agosti 15, 2019.

Kwa mujibu wa barua ya Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), Padre Charles Kitima imesema nafasi ya Kardinali Pengo imechukuliwa na Askofu Mkuu Mwandamizi Yuda Ruwa’ichi.

“Askofu Mkuu Yuda Ruwa’ichi OFM Cap ambaye mpaka sasa ni Askofu Mwandamizi ndiye anachukua rasmi majukumu ya kuliongoza Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam,” amesema Padre Kitima.

Askofu Mkuu Yuda Ruwa’ichi ni kati ya wanafunzi wa Kardinali Pengo aliowahi kuwafundisha wakati alipokuwa akifanya kazi hiyo katika seminari ya Kipalapala iliyoko Jimbo Kuu la Tabora.

Kardinali Pengo alianza kufundisha seminari hiyo mwaka 1977 baada ya kurejea toka Roma alikokuwa ameenda kujiendeleza kwa masomo ya juu katika masuala ya maadili.

Pia Soma

Januari 22, 1990 Kardinali Pengo aliteuliwa kuwa askofu mwandamizi wa Dar es Salaam na mwaka 1992, Kardinali Laurean Rugambwa alipojiuzulu, akawa Askofu Mkuu wa jimbo hilo.

Chanzo: mwananchi.co.tz