Vatican.Kanisa Katoliki limeyafafanua leo matamashi ya Papa Francis kuhusu kile alichokiita kuwa ni utumwa wa ngono katika shirika moja la watawa la kifaransa, likisema kuwa alimaanisha matumizi mabaya ya madaraka ambayo yalionekana katika matukio ya unyanyasaji wa kingono.
Papa Francis amesema hayo akilijibu swali kuhusu unyanyasaji wa kingono unaofanywa na mapadri dhidi ya watawa wakati wa kikao cha waandishi wa habari aliporejea nyumbani kutoka Umoja wa Falme za Kiarabu.
Ilikuwa ni mara ya kwanza ya kwa Papa Francis kukiri hadharani kuhusu tatizo la mapadre na maaskofu kuwanyanyasa kingono watawa.