Dini

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kaimu katibu Bakwata Dodoma afariki dunia, Shekh amlilia

92401 Pic+bakwata Kaimu katibu Bakwata Dodoma afariki dunia, Shekh amlilia

Mon, 20 Jan 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Kaimu katibu mkuu wa Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata) Mkoa wa Dodoma, Twaha Mwaya amefariki dunia jana Jumapili Januari 19, 2020 katika Hospitali ya Rufaa mkoani humo alikokuwa akitibiwa baada ya hali yake kudhoofu.

Mwili wa Mwaya utazikwa leo Jumatatu Januari 20, 2020 katika makaburi ya Kwamwatano yaliyoko Maili mbili jijini Dodoma.

Sheikh wa mkoa wa Dodoma, Alhaji Mustafa Rajab Shabani amesema mtendaji huyo ameondoka na kwao wanaona mti mkubwa uliodondoka na kuacha kishindo lakini akabainisha yote ni mapenzi ya Mungu.

“Innaa lillahi wainnaa ilaihi raajiuun. sisi ni wa allah na kwake allah tutarejea. nachukua fursa hii adhwiim kwa moyo ulojaa majonzi  na wenye kuamini qadari za allah,” alisema Shekh Rajabu.

Alhaji Rajabu ametaja sababu za kifo cha Mwaya kuwa alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa moyo kwa muda mrefu na shinikizo la damu ambalo lilisababisha mauti kumkuta.

Katika uhai wake, Mwaya alikuwa Katibu wa Bakwata wilaya ya Dodoma na alikuwa na ushawishi na muumini wa amani kwani katika vikao alivyohudhuria alizungumzia amani na upendo wakati wote.

Pia Soma

Advertisement
Kwa mujibu wa Alhad Rajab, Bakwata Dodoma imepoteza mtu muhimu waliyekuwa wakimtegemea kwa sehemu kubwa katika kuwaunganisha waumini na hakuwahi kuwa na ubaguzi.

Kiongozi huyo amewataka waumini na wakazi wa Dodoma kutulia katika kipindi hiki wakati wakitafuta  kwa sehemu kubwa alifanya kazi kwa kutumikia nafasi mbili kwa wakati mmoja.

Chanzo: mwananchi.co.tz